- Kitoloho
Headlines News :
Home » »

Written By Msamaa on Tuesday, May 7, 2013 | 11:24 AM

…FBI watua kuchunguza
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo
ASKARI wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), wamewasili mjini Arusha jana asubuhi kwa ajili ya kuongeza nguvu za kuwasaka watu waliohusika na mlipuko wa bomu katika Kanisa la Parokia ya Joseph Mfanyakazi Olasite. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo waliwaambia hayo wananchi eneo hilo jana jioni, wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwatembelea kwa ajili ya kuwapa pole waumini wa kanisa hilo.
“Ndugu zangu, nawapa pole sana, Serikali yenu inakesha usiku na mchana, napenda kuwaambia leo (jana) tumepokea askari wa FBI hapa kwetu wamekuja kuongeza nguvu ya kuwasaka wahalifu hawa.

“Tunawaomba mwendelee kutusaidia kwa kila aina na taarifa zenu tutazifanyia kazi muda wote, tutahakikisha wote waliohusika wanatiwa mbaroni,” alisema Mulongo.

Kwa upande wake, Pinda alisema amesikitishwa na tukio hilo ambalo mpaka jana jioni limesababisha vifo vya watu watatu.

Alisema kwa wale wote ambao wamefariki, Serikali itagharamia mazishi yao kwa gharama na watazikwa kwa heshima zote zinazotakiwa.

“Nimemwagiza RC Mulongo, kuhakikisha wanafuatilia wale wote ambao wamefariki wanazikwa kwa gharama zote za serikali.

“Pia nimemwagiza ahakikishe majeruhi wote wanaendelea kutibiwa kwa gharama za Serikali na hata wale ambao wameruhusiwa kwenda majumbani mwao, wafuatilie ili kujua wanaendeleaje,” alisema Pinda.

Alisema taarifa alizonazo, ni kwamba majeruhi mmoja aliyekuwa akikimbizwa kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu alifia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

“Majeruhiwa wengine 24, wameruhusiwa kwenda nyumbani na wengine wanaendelea na matibabu.”

Alisema hadi jana jioni, polisi walikuwa bado wanamshikilia mtuhumiwa mmoja, Victor Ambrose (20), ambaye anadaiwa kuwa alirusha bomu hilo.

“Mpaka leo (jana), kuna Victor Ambrose anashikiliwa na polisi, nawashukuru watu wote waliomfukuza na kumkamata baada tu ya tukio hili kutokea,” alisema Pinda.

Alisema Serikali katika tukio hili, kamwe haitakwepesha ukweli na itatoa taarifa zote kwa wananchi.

Naye Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa (CCM), aliwaambia waumini hao kuwa Yesu alikufa msalabani na mwisho wa siku alifufuka na kushinda dhambi na mauti.

SOURCE:MTANZANIA.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

ZILIZOSOMWA SANA.

Followers

Blog Archive

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Kitoloho - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template