- Kitoloho
Headlines News :
Home » »

Written By Msamaa on Thursday, May 2, 2013 | 7:08 AM

Mtihani darasa la saba 1998:
Manispaa Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki
  • Wazazi Waislamu wapigwa na bumbuwazi
  • Walimu wakuu watuhumiwa
Na Rajab Rajab, Morogoro
WASI WASI mkubwa umeanza kuwaingia wazazi Waislamu wa mjini hapa kufuatia kupatikana kwa barua kutoka ofisi ya Elimu Manispaa inayowaagiza walimu wakuu wote wa shule za msingi kupeleka majina ya wanafunzi Wakatoliki wa darasa la saba wa mwaka huu.
Mapema juzi baadhi ya Waislamu walionekana kupigwa na bumbuwazi
baada ya kupata taarifa hizo na baadhi yao wakiwa wameiona nakala ya barua hiyo.
 
Gazeti hili lilifanikiwa kuipata nakala ya barua hiyo ambayo imetiwa saini na mtu aitwaye E.P. Mpessa kwa niaba ya Afisa Eimu wa Manispaa ya Morogoro.
Katika barua hiyo yenye kumbukumbu namba E.10/MMC-1/183 iliyoandikwa Juni 9 mwaka huu, inawataka walimu wakuu wote wa shule za msingi Manispaa ya Morogoro kutuma majina ya wanafunzi Wakatoliki darasa la saba hadi kufikia Juni 12, 1998.
 
Barua hiyo fupi haikufafanua kiundani majina hayo ni ya nini jambo ambalo limewafanya Waislamu wa hapa kuanza kuwatilia mashaka walimu wakuu wa shule hizo kuwa wanafahamu suala hilo kiundani zaidi ndio maana Mwandishi hakulazimika kufafanua.
Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya Waislamu wamedai kuwa vitu vya namna hiyo ndivyo vinavyowafanya waumini wa dini ya Kiislamu kuituhumu serikali kuwa inawapendelea Wakristo katika nyanja zote na hususan katika elimu.
"Hali hii na mikakati kama hii viongozi wetu wa Kiislamu walio serikalini hawajui na wakipewa taarifa kama hii huwa hawaifanyii kazi badala yake wanawarushia Waislamu kashfa kwa kuwaambia hawana dira", alisema kwa uchungu muumini mmoja wa eneo la Kingo Bwana Ally Seifu.
Naye Bw. Athman Salim wa Mafiga amesema "hata watoto wetu wasipochaguliwa kujiunga na shule za sekondari za serikali mwakani tutaamini kuwa imetokana na njama hizi."
 
Kufuatia kupatikana waraka huo baadhi ya waumini wametishia kulipeleka suala hili mbele ya sheria (mahakamani) kwa madai kuwa linahatarisha hali ya baadaye ya vijana wao kimasomo.
Aidha baadhi ya waumini hao wa Kiislamu wameiomba serikali kutopuuzia hali hii na kwamba ufanyike uchunguzi wa kina kwa kuunda tume huru vinginevyo huenda kukatokea mgawanyiko miongoni mwa raia wake.
Mitihani ya Darasa la Saba inatarajiwa kufanyika nchi nzima mwezi Septemba mwaka huu.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

ZILIZOSOMWA SANA.

Followers

Blog Archive

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Kitoloho - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template