- Kitoloho
Headlines News :
Home » »

Written By Msamaa on Thursday, May 2, 2013 | 4:26 AM


Pinda awaangukia viongozi wa dini
 
na Happiness Mnale {TANZANIA DAIMA , May 2, 2013}
 
SERIKALI imewaomba viongozi wa dini kusisitiza amani kwa waumini wao kutokana na viongozi hao kumiliki kundi kubwa la jamii ambalo linawasikiliza, kuwaamini na kutekeleza maelekezo yao.
Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika ibada ya misa ya kuwekwa wakfu Askofu msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Titus Mdoe.
Alisema kuwa kwa vile Kanisa Katoliki linaadhimisha Mwaka wa Imani, ni vyema maaskofu wakatumia nafasi na kipindi hicho kuwaimarisha waumini wao kiimani na hatimaye kuwa mfano kwa jamii.
Alisema kuwa Tanzania kwa sasa inapitia changamoto za kisiasa, kijamii na utawala, hivyo ni vyema viongozi wakasimamia kwa karibu maadili mema katika jamii yanayohitaji upendo, busara na hekima.
Pinda aliongeza kuwa changamoto nyingine ni vuguvugu la ukosefu wa amani na utulivu katika baadhi ya maeneo nchini, hali inayosababisha kuwepo na ishara ya uadui baina ya wananchi ikiwemo udini na ukabila.
Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Francisco Padilla, alimtaka Askofu Mdoe kulilea kanisa, kufanya kazi kwa karibu na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, ambaye ni Askofu Mkuu wa jimbo hilo kutokana na uzoefu alionao.
Pia alisema kuwa askofu huyo msaidizi amechaguliwa kutokana na uwezo wake kiutawala na kumtaka kuwa karibu na Mungu na kuendelea kuyatoa maisha yake kwa ajili ya kanisa.
Kardinali Pengo naye alimtaka askofu Mdoe aendeleze azimio la kuhifadhi imani na kujenga mwili wa Kristo na kusimamia masuala ya mawasiliano, uchungaji, litrujia, vijana, vyama vya kitume, katumene, afya na majadilino ya kidini.
Askofu Titus Mdoe alizaliwa miaka 52 iliyopita, na alipata daraja la ushemasi Desemba 3, 1985 na kupadrishwa Juni 24, 1986 na anaungana na muhashamu Askofu Euzebius Nzigilwa kumsaidia Kardinali Pengo.
Mbali na Pinda pia walihudhuria marais wastaafu, Benjamini Mkapa na Ali Hassan Mwinyi, mawaziri wakuu wastaafu, mawaziri, viongozi wa dini mbalimbali na wanasiasa.

 
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

ZILIZOSOMWA SANA.

Followers

Blog Archive

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Kitoloho - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template