- Kitoloho
Headlines News :
Home » »

Written By Msamaa on Friday, May 3, 2013 | 1:21 PM

RAIS KIKWETE AMTEUA BALOZI MANONGI KWENDA UN

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Tuvako Manongi kuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York.

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatano, Julai 25, 2012 na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Bwana Peniel Lyimo kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Dar es Salaam imesema kuwa uteuzi huo ulianza jana, Julai 24, 2012.

Kabla ya uteuzi wake, Balozi Manongi ambaye ni ofisa wa miaka mingi wa masuala ya nchi za nje, alikuwa Mshauri Mwandamizi katika Ofisi ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, New York.

Balozi Manongi anachukua nafasi ya Balozi Ombeni Y. Sefue ambaye aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi Desemba 30, mwaka jana, 2011.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
25 Julai, 2012
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

ZILIZOSOMWA SANA.

Followers

Blog Archive

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Kitoloho - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template