Pengo awatoa hofu waumini, ataka waendelee kusali. - Kitoloho
Headlines News :
Home » » Pengo awatoa hofu waumini, ataka waendelee kusali.

Pengo awatoa hofu waumini, ataka waendelee kusali.

Written By Msamaa on Monday, May 20, 2013 | 12:34 AM


CHANZO:MWANANCHI.



Top of Form



Bottom of Form

Posted Jumapili,Mei19 2013 saa 21:8 PM

Dar es Salaam.

Askofu wa Kanisa Katoliki,Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewataka waumini wa kanisa hilo kutoogopa kifo badala yake waendelee kwenda makanisani licha ya kuwapo kwa vitisho vya kushambuliwa.

Pengo alisema hayo jana katika Kanisa la Mtakatifu Joseph alipokuwa akitoa sakramenti ya kipaimara na aliwataka wasiwe na hofu lakini waendelee kumwamini Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu.

“Tuendelee kwenda makanisani,kamwe tusiogope kuuawa,tuwe na imani kwamba Yesu Kristo ndiye mlinzi wetu na ndiye atuongozaye,”alisema Pengo.

Kardinali Pengo alisema hata kama vyombo vya dola vitakuwa vimeshindwa kuwalinda,waumini kamwe wasiache kwenda makanisani kwa ajili ya kuabudu.

Pengo aliwataka waumini hao kutolipiza kisasi kutokana na mauaji yaliyotokea hivi karibuni mkoani Arusha kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na mafundisho ya Yesu Kristo.

“Wakristo kulipa kisasi ni kwenda kinyume na mafundisho ya dini ya kikristo na sheria za nchi,” alionya Pengo.

Kauli hiyo imekuja baada ya watu watatu kuuawa kwa bomu na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa hivi karibuni katika Kanisa Katoliki,Parokia ya Joseph Mfanyakazi,Olasiti nje kidogo ya jiji la Arusha.

Mauaji hayo yalitanguliwa na kuuawa kwa Padri Evarist Mushi aliyeuawa Februari 17 wakati akielekea katika Kanisa la Mtakatifu Theresia,Zanzibar kuendesha misa.

Pia Desemba 25 mwaka jana,Padri Ambrose Mkenda alijeruhiwa baada ya kupigwa risasi watu wasiojulikana wakati akisubiri kufunguliwa geti nyumbani kwake Zanzibar.

Pengo aliwataka waumini wote kuendelea kusali kwa imani yao na kwamba matatizo yanayojitokeza yasiwakatishe tamaa.

Alisema hata katika mafundisho, kuna mambo mengi ambayo yalifanywa na baadhi ya watu ili kumkatisha tamaa Yesu Kristo asitimize malengo yake lakini baadaye alishinda.

“Vivyo hivyo waumini yanayojitokeza hivi sasa yasitukatishe tamaa tuendelee na utaratibu wetu wa siku zote na tutashinda,”alisema Pengo.




Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

ZILIZOSOMWA SANA.

Followers

Blog Archive

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Kitoloho - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template