- Kitoloho
Headlines News :
Home » »

Written By Msamaa on Thursday, May 2, 2013 | 4:51 AM


 

Ujumbe wa Mufti watua kwa maaskofu.
 
na Mwandishi wetu{ TANZANIA DAIMA , May 2, 2013}
TIMU iliyoundwa na Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Shaaban Simba, kuzungumza na Wakristo ili kuondoa tofauti kati ya Wakristo na Waislamu na kujenga ushirikiano imeanza kazi yake jana.
Timu hiyo imeanza kazi kwa kupeleka waraka maalumu ulioandikwa na Mufti na kufanya mazungumzo ya faragha na maaskofu ambao ni viongozi wa Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste nchini (CPCT).
Waraka huo uliopokewa na Katibu Mkuu wa CPCT, Askofu Dk. David Mwasota, kwa niaba ya maaskofu wa umoja huo, utajadiliwa na kutolewa uamuzi.
Alisisitiza kuwa jambo alilolifanya Mufti ni jema na la kihistoria, ambalo lina nia ya kuleta amani na maelewano ya kudumu baina ya wanadini nchini.
“Tumepokea wawakilishi wa Mufti (ujumbe wa timu yake) na waraka maalumu kutoka kwa Mufti mwenyewe. Ujumbe wake una lengo la kutaka kukutana na sisi, kwa lengo la kuzungumza na kuondoa tofauti ambazo zimekuwa zikijitokeza.
“Hivyo tumeupokea na tutaufanyia kazi kwa pamoja na nina hakika tutaukubali wito wake kwa kuwa una nia njema, kwa maslahi ya nchi yetu na watu tunaowaongoza,” alisema Askofu Dk. Mwasota.
Kwa upande wake timu iliyoundwa na Mufti imesema, suala la kulinda na kudumisha uhuru wa kuabudu, maelewano, amani na usalama wa jamii ni wajibu wa kila raia.
Hivi karibuni Mufti Mkuu wa Tanzania, Shaban Simba, alitangaza kuunda timu hiyo ya masheikh na wanazuoni wa Kiislamu, itakayotafuta maridhiano baina ya Wakristo na Waislamu ili kudumisha uhuru wa kuabudu, amani na usalama nchini.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

ZILIZOSOMWA SANA.

Followers

Blog Archive

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Kitoloho - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template